Translate this blog in your favourable language

My pager view

Thursday, January 11, 2018

ZIFAHAMU TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI WA KUKU KUANZIA VIFARANGA NA KUKU WAKUBWA.

Mtaalam wa Mifugo akiwapa chanjo vifaranga.


Kuku wakienyeji ni rahisi sana kuwafuga tofauti na wakisasa.

Chanjo kama hii mfugaji unaweza kuchanja kwa maelekezo ya wataalam.

Zipo namna nyingi za uchanjaji wa kuku zingine zinahitaji utaalam

TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI
    Wakati wa kutayarisha mpango wa kuchanja kuku kwa ajili ya kinga dhidi ya magonjwa, kuna vipengele vikuu sita Ambavyo unatakiwa uvifahamu na kuvizingatia. Vipengele hivyo ni kama ifuatavyo:

1. Vifaranga vinavyoanguliwa kwa pamoja:
 Iwapo una kundi zaidi ya moja la vifaranga wanaoanguliwa,
Weka utaratibu wa chanjo ambao utapunguza uwezekano wa magonjwa kuenea shambani. Hivyo basi,
Hakikisha vifaranga na kuku wote wanapata chanjo kwa pamoja.
2. Umri wa kuchanja kuku:

IJUE NYUMBA YA KULELEA VIFARANGA WA SIKU 1 HADI WIKI 4 KITAALAM [MWONGOZO KWA MFUGAJI WA KUKU]

Cage maalum ya kukuzia vifaranga wachache..

Sehem maalu imezungushiwa wigo kwa ajili ya kulea vifaranga kwa kutumia taa za umeme.
Sehemu unayoweza kulea vifaranga kwa maeneo ya wazi na maeneo ya Baridi na hata kuku wakubwa unaweza kuwalea katika nyumba kama hii.

Hii ni nyumba ya wafanyabiashara wakubwa ama makampuni yanayojishughulisha na uleaji vifaranga..

Utangulizi

      Kwa kawaida au katika hali halisi, kazi ya kulea vifaranga hufanywa kuku mwenyewe. Hivyo
ili kulea vifaranga, mfugaji ni lazima aige kuku anavyofanya. Ikumbukwe kuwa vifaranga
husumbuliwa zaidi na hali mbaya ya hewa, magonjwa mbalimbali, kukosa chakula kisichofaa
na kukosa uangalizi wa karibu.
     Ni lazima vifaranga waangaliwe kwa kuwapatia nyumba yenye joto, chakula kinachofaa
na maji safi , kuwakinga dhidi ya magonjwa masumbufu kwenye eneo husika na kuwatibu
wanapougua. Mfugaji anayefanikiwa ni yule anayelea vifaranga wenye afya nzuri ambao
hatimaye hutoa mazao mengi yanayompa faida.