Translate this blog in your favourable language

My pager view

Tuesday, April 10, 2012

NA HII NDIO ILIKUWA SAFARI YA MWISHO YA STEVEN KANUMBA.

katika hali ambayo mimi niliitegemea kabisa ni mkusanyiko usio na mfano katika safari nzima ya kumsindikiza Steven Kanumba katika safari yake hii ya mwisho ambyo iliambatana na msongamano mkubwa watu hali iliyohatarisha pia maisha ya watu lakini hakuna madhara hasa ya watu kufa ila wengi walizimia kutokana na hali mbalimbali ikiwemo majonzi na msongamano na kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa mooa amesema hakuna aliyeripotiwa kufa kutokana na mkusanyiko huo

na yafuatayo ni matukio katika picha kuhussiana na safari hiyo tangu leaders mpaka makaburuni kinondoni makaburini na baadhi ya picha ni kutoka katika mitandao tofauti.

Hapa wakijiandaa kutumbukiza mwili wa kanumba kaburini katika makaburi ya kinondoni

Swahiba wa karibu wa Kanumba[ Ray] alukuwa akishuhudia kwa karibu hatima ya rafiki yake kipenzi


hapa jeneza likiandaliwa kuwekwa kaburini

baadhi ya watu wakitoa heshima zao za mwisho katika mazishi ya kanumba

kulingana na idadi kubwa ya watu ulinzi uliimarishwa kila pande kuhakikisha kuwa watu wanakuwa na amani mda wote

baadhi ya wasanii waliowahi kuogiza na kanumba wakiwasili eneo la tukio kwa ajili ya mazishi

hiki ndicho chumba ambaco ndani yake amelala kanumba the greate

watu mashuhuri wakitoa heshima zao za mwisho kama ambavyo inaonekana

mama wa kanumba akiwapungua mkono walihudhuria katika mazishi ya mwanae kanumba

jeneza la kanumba likiwasili viwanja vya leaders mapema leo likiwa limebebwa na wasanii wenzake

Hemedi na Mlela wakiwasili viwanja vya leaders

hali haikuwa hali leaders wengi walizimia na ililazimu kazi ya ziada kwa wahudumu wa msalaba mwekundu

mama Salma kikwete akitoa heshima zake za mwisho viwanja vya leaders leo

kamanda Kova akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa kanumba mapema leo

jeneza la kanumba likiwasili leviwanja vya leaders mapema asubui leo likiwa limebebwana wsanii wenzake akiwemo Issa musa Cloud na wengine.
                      Leo ndio ilikuwa siku ya mwisho ya kumsindikiza Kanumba katika makao yake ya milele na hakika daima atakumbukwa kwa mengi na pengo lake wakuliziba simuoni ila cha msingi ni kuendeleza yale mema yote aliyoyafanya katika ulimwengu huu.
                  MUNGU AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA STEVEN KANUMBA
                                                                             AMEN. 

Monday, April 9, 2012

Hii ni taarifa ya kamanda wa pilisi na maelezo mafupi ya lulu na RATIBA YA KUMSINDIKIZA HAYATI STEVEN KANUMBA.


HATIMAYE LULU AZUNGUMZA ASEMA HAKUMSUKUMA KANUMBA Baada ya kugoma kutoa maelezo kwa takribani siku nzima ya jana, mwanadada Lulu hatimaye amezungumza na polisi na kuelezea kilichotokea baina yake na marehemu Steven Kanumba. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema Kanumba alikufa kutokana na u...gomvi uliotokea kati yake na rafiki yake wa kike Lulu. "Kanumba amefariki usiku wa kuamkia leo (jana) majira ya saa tisa usiku, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ugomvi kati yake na rafiki yake wa kike anayejulikana kwa jina la Elizabeth Michael 'Lulu' mwenye umri wa miaka 18. Alisema kabla ya ugomvi huo kutokea kati yao wakiwa chumbani, simu ya Lulu iliita na akaamua kutoka nje kupokea kitendo kilichomuudhi Kanumba. Kamanda Kenyela alisema Kanumba aliamua kumfuata Lulu nje huku akifoka kwa sauti akitaka aelezwe kwanini alitoka nje kupokea simu huku akimtuhumu kuwa huenda alikuwa akizungumza na mwanaume mwingine.
 Aliongeza baada ya Lulu kuona Kanumba akimfuata aliamua kukimbia kutoka nje ya geti , lakini kabla hajafanikiwa kufungua geti, Kanumba alimkamata na kumrudishwa ndani. Kamanda Kenyela, alisema Kanumba akiwa amemshikilia waliingia wote chumbani na kufunga mlango. Hata hivyo, alisema haijulikani nani aliyefunga mlango, ingawa maelezo ya Lulu anadi kuwa aliyefunga mlango ni Kanumba. Kamanda huyo alisema Lulu anaeleza kuwa baada ya Kanumba kufunga mlango, alimuona akilegea na kujigonga kisogo chake kwenye ukuta wa chumba hicho kabla ya kuanguka chini. Alibainisha kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Kanumba alikuwa amekunywa Whisky (pombe kali) aina ya Jacky Daniel, hata hivyo, bado wanachunguza zaidi kujua kama kweli Kanumba alilegea tu na kuanguka, ama alipigwa na kitu kizito kichwani au alisukumwa kwa nguvu na kumfanya aangukie kisogo. “Uchunguzi ukikamilika tutampeleka mahakamani kwa tuhuma za mauaji,” aliongeza Kamanda Kenyela.

Steven kanumba aliyefikwa na mauti usiku wa kuamkia jumamosi atazikwa kesho jijini dar es salam katika makaburi ya kinondoni kama amabvyo familia na wadau walivyopendekeza azikwe jiji dar. Kamati ya mazishi inayoongozwa na Mtitu ilitoa taarifa ya ratiba hiyo na ratiba hiyo iakuwa ni kama ifuatavyo.
                                                                RATIBA KAMILI.

Mwili wa marehemu Steven Kanumba utachukuliwa kwa msafara kutoka Hospitali ya Taifa, Muhimbili saa 2:30 asubuhi. Utapitishwa Barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi hadi Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni ambako Misa ya kumuombea itasomwa pamoja na salamu mbalimbali kabla ya watu wote kumuaga.

Wito unatolewa kwa watu kujitokeza kwa wingi kuanzia saa 2:00 asubuhi, wakijipanga kando ya Barabara za Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi ili wautolee heshima mwili wa Kanumba wakati ukitolewa Muhimbili kwenda Leaders Club.
Saa 3:30 asubuhi, mwili wa Kanumba utapokelewa Viwanja vya Leaders, ukitanguliwa na mapokezi ya wazazi wake, viongozi mbalimbali wa serikali ambao juu yao kabisa atakuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohamed Gharib Bilal.
Saa 4:00, itakuwa ni muda wa kusoma Misa ambayo itachukua dakika 60, saa 5:00 kitakuwa kipindi cha salamu kutoka kwa watu mbalimbali.
Saa 6:00 mchana, ratiba ya kumuaga Kanumba itaanza mpaka saa 9:00 alasiri na baada ya hapo, utakuwa wakati wa kuusafirisha mwili kwa msafara kutoka Leaders Club mpaka Makaburi ya Kinondoni, msafara ukipita Barabara ya Tunisia, utakatisha Barabara ya Kinondoni kuelekea makaburini.
Saa 10:00 alasiri, mazishi yatafanyika kwa kufuata utaratibu wa imani ya marehemu.
Kamati ya Mazishi inatoa wito kwa watu watakaohudhuria shughuli ya kumzika ndugu yetu Kanumba, kuja na maua ili kumuaga kwa heshima.
Utulivu, unyenyekevu na ustahimilivu ni mambo muhimu yanayohitajika katika kipindi chote cha kumuaga mpendwa wetu Kanumba.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Sisi wote tulimpenda kwa dhati na tulitamani aendelee kuwa nasi siku zote ila Mungu aliyemleta kwa mapenzi yake ameamua kumchukua. Jina lake lihimidiwe.

        K.N.Y GABRIEL MTITU
     MWENYEKITI WA KAMATI YA MAZISHI

Saturday, April 7, 2012

REST IN PEACE WAJINA STEVEN KANUMBA [Matukio ya msiba katika Picha] WE ARE BACK YOUR

Mama wa Kanumba Flora Mwitegoa
Mama wa kanumba  awasili jijini dar es salam na pia adhibitisha kuwa mwanae atazikwa dar na atazikwa
 katika makaburi ya kinondoni siku ya jumanne.
                                 Steven kanumba na mama yake kushoto na Dotnata kulia

mama wa kanumba ( Flora Mutegoa) akiwa na huzuni kubwa baada ya kumpoteza mwanaye kipenzi Steven kanumba
Katika mahojiano yaliyofanyika Mama mzazi wa Steven Kanumba amesema angependekeza mwanaye azikwe jijini Dar es salam na aliskanusha taarifa kuwa mwanaye hana ndugu kwani yeye ndiye mama yake na kuna dada yake pia wapo ndugu wengi sehemu mbalimbali hapa Nchini.  na Taarifa zingine zinasema kuwa Lulu amekataa kutoa ushirikiano kwa Polisi Mpaka pale Mwanasheria wake atakapofika bado taarifa ya madaktari inasubiriwa na pia taarifa ya kipolisi kuhusiana na kifo cha Steven Kanumba Pichani hapo chini.

Tabasamu hili natumai utaingia nalo huko uliko kwasasa but duniani umetuachia simanzi kubwa sana kama kuna uwezekano wa kuwaona wasalimie Mzee kipara, mr Ebbo, complex na Vivian, john mjema, steve 2k, faza nelly nk.

baadhi ya watu maarufu na wanchi ndugu jamaa na marafiki walifika sinza kuwafariji waliofikwa na msiba huu mzito

Kila mmoja alikuwa anawaza lake na alikuwa na huzuni  kwa namna yake ni wazi msiba huu umemgusa kila mtu hasa kutokana na ughafra wake.

wasanii wengi walikuwepo Natasha ambaye walikuwa wote kaole na katika filamu nyingi walikuwa ni moja ya wahudhuriaji msibani hapo

wananchi wa jiji la Dar er salam walifurika nyumbani kwa Kanumba kwa ajili ya kujua kinacho endelea msibani hapo

Hapa ndipo palipokuwa nyumbani kwa kanumba ambapo mauti yalimkuta akiwa katika nyumba hii

mke wa waziri mkuu akisaini kitabu cha rambirambi na pia kuwafariji wale wote waliofikwa na msiba huu mzito kabisa.

Samweli 6 pia alikuwepo katika msiba huu mzito. na pia walikuwepo mamia ya wakazi na maeneo ya jirani na dar es salam

 xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Taarifa zilizopo mtaani kwa sasa ni kuhusu kifo cha msanii wa maigizo na filamu nchini tanzania namzungumzia Steven kanumba amabye katika hali ya kushtua sana nilipata taarifa za kifo chake kutoka kwa rafiki yangu wa karibu mida ya saa kumi alfajiri ya leo na kwakweli nilipata mshtuko mkubwa na ilinikumbusha sana kifo cha marehemu kaka yangu amabye nae alifariki mida ambayo kanumba alifariki na ilikuwa ni ghafra sana kama ambavyo kimetokea kifo cha kanumba. Chanzo cha kifo cha kanumba mpaka sasa bado ni kitendawili ambacho wengi hatukufahamu ila kwa taarifa ambazo sio rasmi sana ki ugomvi wa mapenzi baina yake yeye na mpenzi wake Lulu taarifa hizo pia zinzfafanua kuwa Kanumba alianguka na kuumia kichwani baada ya mpenzi wake ambae anatajwa kuwa ni mwigizaji LULU(Kwa sasa msanii wa kike Lulu pichani anashikiliwa na police kwa maelezo zaidi) 
kumsukuma na kuanguka wakati wanagombana.
‘Inasemekana’ Kanumba wakati akijiandaa kutoka saa sita usiku aliingia bafuni kuoga, alipotoka alimkuta Lulu akiongea na mwanaume mwingine kwenye simu ndipo alipokasirika na ugomvi kuanza.
Alipelekwa hospitali Muhimbili ambako muda mfupi baadae alifariki dunia, mwili wake bado uko katika chumba cha kuhifadhia maiti Muhimbili hospital.
pia inaaminika kuwa 
chanzo cha kifo chake ni baada ya kuanguka na kuanza kutoa mapovu hapohapo nyumbani kwake, alikua akiishi na mdogo wake anaitwa Fetty aliekua chumba kingine ambae amethibitisha kweli kwamba alimkuta kaka yake akiwa ameanguka.
Polisi wameondoka nyumbani kwa Kanumba muda mfupi uliopita baada ya kuwachukua waliokua wanaishi na Kanumba akiwemo mdogo wake Fetty ili kwenda kusaidia maelezo ya kilichotokea.

 haya ni mambo ya mwisho kuyandika kanumba katika face book na twitter hii ni kutoka millard ayo website.na baadhi ya maoni ya watu kupitia facebook









na hii ni post au habari yake ya mwisho katika blog yake ya kanumba the great. ambayo ameiandika jana april 6 2012.

HAPPY 5TH ANNIVERSARY TMH,SAMBAMBA NA UZINDUZI WA DUKA/OFISI & TRAINING CENTER

SEHEMU YA DUKA LA NGUO TOKA KWA DESIGNER MBALIMBALI.
TULIOSAPOTI MPAKA KITUO HIKI KUFIKIA HAPA KILIPO SOMA MAJINA HAPO JUU JINA LANGU LIPO HAPO,KUSEMA UKWELI INAPOKUJA MAMBO YA KUSAIDIA JAMII NAJITAIDI KUTOA NINACHOKUA NACHO MAANA HAPA HUKUMBUKA MANENO YA MWANDISHI ALBERT PINE..''"What we do for ourselves dies with us. What we do for others and the world remains and is immortal."
'' KANUMBA THE GREAT PIONEER MOTO WA VOLCANO'' NIKIWA KTK OFISI ZA TANZANIA MITINDO HOUSE.
Pia amecheza filamu nyingi na maigizo mengi katika kundi la kaole sanaa group na hizi ni filamu chache alizo cheza Steven Kanumba.
    JOHARI, DAR TO LAGOS, THA BIG DADDY, MOSES, SHE IS MY SISTER, BECAUSE OF YOU, DEVIL KINGDOM, THIS IT IS, MORE THAN PAIN,OFF SIDE,UNCLE JJ,DECEPTION, THE SHOCK, NK. 


 BAADHI YA WASANII NA WATU MAARUFU WAMIMINIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU WAKIWA NA MAJONZI MAKUBWA. picha na dj choka.
swahiba mkubwa wa Knumba Ray

baadi ya waigizaji na wasanii wafilamu wakiwa na majonzi

huzuni imetawal kwa kila mmoja najua hata wee imekugusa.

baadhi ya wasanii wa maigizo na filamu.


maoni ya wadau mbalimbali na watu maarufu yazidi kumiminika 
haya yalikuwa ya zitto kabwe.....mungu amekuchukua mapema sana. Umetuachia majonzi makubwa mno. Tangulia. Tuwekee nafasi huko. Kungekuwa na rufaa.......... 
haya yalikuwa ya salama jabir......Rest In Peace Steven...M/Mungu Alikupenda Zaidi. Rest In Peace My Brother 
haya yakikuwa ya Happnes Magesse......Rest in Peace my friend...you create jobs ,you believed on our own...and you took them as ur own and give them opportunities to believe on themselves and be who they wanna be and take acting as their career....Where do they go now.....Kanumba!!!? Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi...Pigo la taifa jamani..Poleni Kaole poleni Tanzania...!

haya yalikuwa ya roma mkatoliki.......
Dakika...chache baada ya show yangu ya musoma!! Napata taarifa za huu msiba wa THE GREAT K.A.N.U.M.B.A....sikuamini mpaka nilipopiga simu kwa mmoja wa mtu wake wa karibu na kunijibu huku analia kuwa bro hatunaye kweli na ndo' wao wanatoka muhimbili!!....ni msiba mzito na umewagusa wengi nikiwemo!! Pole sana kaole...pole game 1st quality...pole kwa mpinzani wake mkubwa Ray....pole kwa ben swahiba wake sana....dah pole kubwa kwa pacho mwamba!familia yake Na bongo movie wote...pamoja na watanzania wote!! TUTAKUKUMBUKA KWA MENGI KAKA STEVE.....Tumuombee ndugu ye2 apumzike pema peponi!!na asamehewe dhambi zake!! Oooh kaka umetuacha ukiwa angali mdogo...inauma sana!!
haya yalikuwa ya Solo Thang..........R.I.P STEVEN KANUMBA,,,Mungu amekupenda zaid,,Pole kwa familia na ndugu wa karibu na wapaenzi wa bongo movie kwa ujumla,,,gone too soon Hommie!

haya yalikuwa ua irene Uwoya ..........Kwaheri rafiki wangu wa karibu, kwaheri mwalimu wangu wa filamu.. na hizi zilikuwa ni shutma zake kwa Lulu..SIKU YA JUMATATU NILIANGALIA KIPINDI CHA MIKASI CHA SALAMA NDANI CHANEL 5 AMBAKO LULUA LIKUWA MGENI KATIKA KIPINDI IKO NAKUMBUKA KUNA SHWALIA ALIULIZWA KAMA ANA MPENZI AKAJIBU YEYE BADO NI MTOTO HANA MPENZI LAKINI MUNGU AONGOPEWI HATA SIKU MOJA NI SIKU TANO TU ZIMEPITA SASA MTOTO HUYU ANAUMBUKA KWA KUHUSISHWA NA KIFO CHA STEVEN KANUMBA AMBAYE JIPU LIMEPASUKA KUWA NDIE ALIKUWA MPENZI WAKE JAPO ILIKUWA SIRI SASA YAMEFICHUKA HAKIKA IMENIUMA SANA NAOMBA DOLA IFUATE MKONDO WAKE HUYU MTOTO AADABISHWE.
.

   Alale pema peponi Steven Kanumba bwana ametoa na bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe milele na hii ni safari ya wote ametangulia sisi tupo nyuma yako.. amen

 imeandikwa na Steven mruma na kupitia vyombo vingine vya habari. na taarifa zaidi zitakujia na matukio mbambali mbali kusu kifo cha kipenzi cha watu wajina wangu Steven Kanumba. 
toa maoni yako....










Friday, April 6, 2012

Malawi President Bingu wa Mutharika 'dead': His history.



President Bingu wa Mutharika of Malawi has died, ne of the doctors who treated Mr Mutharika, 78, said the president was "clinically dead" on Thursday after suffering a cardiac arrest. State media has only reported that he has been flown to South Africa for medical treatment.
If confirmed, his death would spark a constitutional crisis, analysts say.
According to the constitution, the vice-president takes over if the head of state is incapacitated or dies in office.
But Vice-President Joyce Banda and Mr Mutharika fell out after a row over the succession in 2010, and she was expelled from the ruling Democratic People's Party (DPP).
Mr Mutharika's brother, Foreign Minister Peter Mutharika, was chosen instead of Ms Banda to be the DPP's presidential candidate in the 2014 elections.
He has been standing in for the president when needed during official occasions. Ms Banda recently told the BBC she had not spoken to Bingu wa Mutharika for more than a year.
The BBC's Raphael Tenthani in the main city, Blantyre, says ministers met all night to discuss the situation.
The doctors and ministers say that Mr Mutharika's body was taken to South Africa while a decision is taken about what to do next.
Government sources have told the BBC that efforts to resuscitate President Mutharika had failed and that an official announcement is being prepared.
'The laws are clear' Former President Bakili Muluzi - a bitter rival to Mr Mutharika - has called on the authorities to make an announcement.
"It's important that the government announces the condition of the president as soon as possible so that the nation is informed," he told journalists.
I am calling for a constitutional order, for continued peace and order. The laws of Malawi are very clear that the vice-president takes over when the president can no longer govern." Mr Mutharika, a former World Bank economist, came to power in a 2004 election, after being backed by outgoing President Muluzi. Soon afterwards, Mr Mutharika left his United Democratic Front (UDF) to form the DPP, after accusing Mr Muluzi and other UDF leaders of opposing his campaign against corruption.
Since being re-elected with a large majority in 2009, critics allege he has demonstrated an increasingly authoritarian streak.
The president has been under mounting pressure to resign, amid accusations of nepotism and economic mismanagement.
The criticism has led to a souring in relations with major foreign aid donors, especially the United Kingdom.
Last year, Mr Mutharika expelled the UK High Commissioner, Fergus Cochrane-Dyet, after a leaked embassy cable quoted the diplomat as saying that the president could not tolerate criticism.
The Malawian leader said he could not accept "insults" just because the UK was his country's largest aid donor.
In response, the UK expelled the Malawian envoy to London and cut direct aid.
Malawi is one of the poorest countries in the world, with an estimated 75% of the population living on less than $1 (60p) a day.
The country has suffered shortages of fuel and foreign currency since the UK and other donors cancelled aid.

                                       THE SHORT  HISTORY OF MR. MUTHARIKA
Bingu wa Mutharika was born Ryson Webster Thom on 24 February 1934 in  Mutharika's parents, Ryson Thom Mutharika and Eleni Thom Mutharika, were both members of the Church of Scotland Mission which later became CCAP. His father was a teacher for 37 years.
Upon completing his primary education in Blantyre, Mutharika obtained a Grade A Overseas School Leaving Certificate at Dedza Secondary School in 1956. In 1964, he was one of the 32 Malawians selected by Hastings Kamuzu Banda (President of Malawi 1961-1994) to travel to India on an Indira Gandhi scholarship for 'fast track' diplomas. The BBC reports that he went to India to "escape then President Hastings Banda's crackdown on political opponents". At some point during the 1960s, he also changed his name, to Bingu wa Mutharika.In India, Mutharika earned his Bachelor's degree in Economics. Subsequently, he attended the Delhi School of Economics graduating with a M.A. degree in Economics. He later obtained a Ph.D. degree in Development Economics from Pacific Western University of Los Angeles, California (USA). Mutharika also completed short courses on Business Management, Financial Analysis, Trade Promotion, Political Leadership, regional Economic Co-operation and Human Relations.
Mutharika served in the Malawi civil service. He has served as Administrative Officer in the Government of Malawi and Zambia. He was offered the Deputy Governorship of the reserve Bank of Malawi and appointed Minister of Economic Planning and Development in 2002.
He worked at the World Bank as a Loans Officer and at the United Nations Economic Commission of Africa, as Director of Trade and Development Finance and as Secretary General of the Common Market for Eastern and Southern Africa COMESA, covering 22 Member States.

News fro BBC and other World media. and edited by Steven mruma.

Thursday, April 5, 2012

NINI CHANZO CHADEMA KUPOKWA JIMBO LA ARUSHA MJINI NA MAHAKAMA?


Katika hali ambayo awali haikutegemewa na wanachi wengi majira ya saa nne asubuhi mahakama kuu mjini arusha ilimuondoa mbunge wa arusha mjini Godbless lema kwa kile kilicho daiwa kuwa ni kutumia lugha ya matusi katika kampeni zake na kuongea lugha za uchochezi ambazo zingeweza kuhatarisha amani ya nchi kitu ambacho ni kinyume na sheria. wengi walijiuliza kama kulikuwa na mono wa mtu lakini kwa mujibu wa mahakama katika mikutan zaidi ya 60 ya kampeni ya Godbless Lema mikutano Nane (8)  alivunja sheria na alitumia lugha za uchochezi, kuna taarifa zilizokuwa zimezagaa baadhi ya mitaa eti aliondolewa katika nafasi hiyo kwasasababu alidanganya uma kuhusu masomo yake ikiwemo vyeti nk.
 lakini baada ya majibu na hukumu ya mahakama alivuliwa ubunge kwasababu ya kutumia lugha chafu na za uchochezi katika kampeni zake wakati akigombea kuingia bungeni mwaka 2010. na wakati huo huo Maandamano ya wafuasi na wanachama wa CHADEMA wakimsindikiza "Aliyekuwa mbunge wao" wa Arusha mjini ndugu Godbless Jonathan Lema kuelekea viwanja vya Ngarenaro majira ya saa 8 na dakika 15 ambapo hatimaye alihutubia wananchi. Mahakama imetengua ubunge wa Lema kutokana na kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa CCM.


Godbless Jonathan Lema amekubali uamuzi wa mahakama na amesema haina haja ya kukata rufaa isipokuwa ATASHINDA TENA kiti hicho katika uchaguzi mdogo utakaoandaliwa na tume ya Taifa ya uchaguzi. kwani bado anaruhusiwa kugombea tena kiti hicho cha ubunge na kwataarifa isiyokuwa rasmi ikulu imekataa kuhusika kwa kuvuliwa kwa ubunge kwa aliyekuwa mbunge wa chadema Godbless lema.