Translate this blog in your favourable language

My pager view

Thursday, December 30, 2010

UZINDUZI WA ALBAMU YA TID WAFUNIKA ZOTE ZA 2010 KAMA ULIKOSA BASI USIKOSE ALBAMU HII YA MFANO.


hapa walioshirikishwa katika wimbo uliobeba jina la albamu wa sifai.
mwanaume wa shoka alieonja ladha ya jela
Kama ulikua bado hujui haya nikwambiayo basi chukua hiyo  huyu ni masanii pekee wa mziki wakizazi kipya namaanisha bongo flava ambae amepitia hatua ya kiume ya kuonja japo kidogo ladha ya jela kama kwa akina 50%, lili wayne, akon nk. namkubali mimi pamoja na watanzania na mamilioni duniani kote na kilichofanya mpaka naamua kuandika makala hii ni uzinduzi wa albamu yake mpya ambao uzinduzi huo naweza nikasema ulikua ni moja kati ya uzinduzi bora kuliko yote ndani ya 2010 nilishuhudia wasanii kibao wakimpa shavu wakiwemo akina ngair, Kelvin mshindi wa big braza 2009 na wasanii wengine kibao na staili alionyoa ilikua ni ya kiubunifu na kama ilikua ya kiduku style laniki alizidi ubunifu na kuwa kivutio kikubwa sana ndani ya billicanas hakika kwangu hakuna kama TID AMBAE NDIE NINAYE MZUNGUMZIA HAPA
HISTORIA NA KIMUZIKI HASA ALIPOTOKA…..
TID katika pozi
Jina lake halisi ni Khalid Mohamed a.k.a TID yaani Top In Dar na si yeye anayejiita hivyo bali wapenzi wake TID  alisoma shule ya msingi Bunge na elimu ya sekondari alienda kuipatia pale Shaban Robert iliyopo ndani ya City la Dsm.
Hapa tid anaelezea historia yake kidogo kimuziki hasa alipotokea  |”nanukuu;;; Unajua tangu niko mdogo nilikuwa napenda sana kusikiliza pamoja na kujaribu kuimba nyimbo
mbali mbali....lakini baada ya kuwa mkubwa na kuanza kujishughulisha na shughuli hizi za muziki ndipo wazazi wangu waliponikumbusha kuwa fanii hii nilikuwa nikiipenda sana toka nipo bwana mdogo ile mbaya hapo ndipo nilipojua kuwa kipaji changu kilianzia mbali sana.

.....Ila nilianza kuimba rasmi mwaka 1996 nilipokuwa nipo shule pale Shaaban Robert nikiwa na wenzangu kama David a.k.a Wabaki, Saitana na Dingo Jango ambapo tulianzisha kundi letu lililoitwa Black Gangster na mara nyingi tulikuwa tukiperfom kwenye concerts za kishule na 'Talent Night ' ambazo tulishinda mara kibao. Yap mwaka 1998 tulirekodi albam iliyojulikana kwa jina la Mission Impossible iliyokuwa na nyimbo 12 na ambazo ziliimbwa kwa 'Ngeli' kimombo mzee hahaha. mwaka uliofuata yaani mwaka 1999 nilishirikishwa kwenye nyimbo ya 'Anza wewe' na kundi la Joint Mobb nyimbo ambayo ilikuwepo kwenye albam yao ya 'Kitinda Mimba'. Vilevile nimeshashirikishwa pia kundi la CBM Crew katika Track yao 'My Girl Friend' na mwaka 
hapa makamuzi ya uzinduzi na AY

2000 nikaanza rasmi maandalizi ya Albam yangu.
Mwaka 2001 Crazy GK akanishirikisha kwenye Track yake 'Tutakukumbuka' na 'Malaika' ambazo zote zinapatikana kwenye albam yake inayokwenda kwa jina la 'Nitakupa Nini Mama' na mwaka huo huo nikafeat na kundi la Taqwa ndani ya nyimbo Maovu na Bongo Chelea Pina na Bongo
Chelea pina ambayo inapatikana katika Compilation ya BNa mwaka huo wa 2001 ndio nikaingia mkataba kama Solo Artist na Studio ya Poa Records iliyo chini ya Producer Amit a.k.a Mental ambapo sasa narekodi albam yangu itakayokuja kwa jina la Sauti ya Dhahabu na itakuwa na jumla ya nyimbo 9 kati ya hizo ni pamoja na Mrembo, Zeze, Hii Mic, Ukweli na nyingine ambazo sitazitaja sasa hivi.ongo Records ya mwaka huo  huyu ndie tid kwa kifupi akielezea wapi hasa alipotoka hapa alikua akikaririwa na media moja hapa Tanzania
logo yake muhimu ya kiburudani
NA KAMA UKIKOSA ALBAMU YAKE UTAKUA UMEKOSA MAMBO MENGI SANA NA UTAKUA BADO HUSTAHILI KUWA MDAU WA MZIKI POPOTE DUNIANI PATA KOPY HALISI UINUE MZIKI WA BONGO NA UMUINUE NA TID KATIKA GEMU… PAMOJA SANA
STEVENN MRUMA